TAZAMA PICHA NA VIDEO MBIO ZA BAISKELI AKINA MAMA WAKIWA NA NDOO ZA MAJI KICHWANI,SHEREHE ZA NANE NANE SHINYANGA CHINI YA UDHAMINI WA TBL
Monday, August 11, 2014
Pichani ni akina mama kutoka katika manispaa ya Shinyanga wakiwa wamebeba ndoo za maji kichwani kabla ya kuanza mashindano ya mbio za baiskeli huku wamebeba ndoo za maji kichwani kuzunguka uwanja wa ccm kambarage Mjini Shinyanga siku ya Sikukuu ya wakulima Nane Nane katika mkoa wa Shinyanga.Mashindano hayo ya mbio za baiskeli yalikuwa yamedhaminiwa na kampuni ya bia Tanzania(TBL) kupitia bia yake ya Safari Lager.
TAZAMA VIDEO HAPA CHINI AKINA MAMA WAKIENDESHA BAISKELI HUKU WAMEBEBA NDOO ZA MAJI KICHWANI KUZUNGUKA UWANJA WA KAMBARAGE
Katika mbio hizo za kuendesha baiskeli huku umebeba ndoo ya maji kichwani mshindi wa kwanza alikuwa Makirikiri Joseph(wa kwanza kulia) ambaye amejinyakulia shilingi laki moja na nusu,mshindi wa pili Christina Giti (katikati)ambaye amepata shilingi laki 1,mshindi wa tatu Joyce Bundala( wa kwanza kushoto) aliyejinyakulia shilingi elfu 80
Mbali na kuandaa mshindano ya mbio za baiskeli kwa akina mama wakiwa wamebeba ndoo kichwani,TBL pia waliandaa mbio za baiskeli kwa watu wenye ulemavu.Pichani washiriki wa mashindano hayo wakijiandaa kuanza mpambano wakizunguka uwanja wa CCM Kambarage mjini Shinyanga
Kulia ni mshindi wa Kwanza Makende Derema aliyejinyakulia shilingi laki 1 na nusu,mshindi wa pili Ngalu Ngamba(katikati) aliyondoka na shilingi laki 1,mshindi wa tatu Peter Thomas( wa kwanza kushoto) aliyejinyakulia shilingi elfu 80
Katika kusherehekea sikukuu ya nane nane mkoani Shinyanga TBL pia waliandaa mbio za baiskeli kwa wanamme za umbali wa kilomita 220.Pichani washiriki wakijiandaa kuanza safari kutoka Uwanja wa ccm Kambarage Shinyanga mjini kwenda Kahama kisha kurudi mjini Shinyanga ,ambapo unaambiwa walitumia masaa 6 na dakika 6 tu
🚧🚦 Usiendeshe gari lako bila Mafunzo na Leseni halali_ 📲 Wasiliana nasi sasa: wa.me/255740273285 Unahitaji nini? 🚘 Unataka kujifunza udereva wa magari na kupata Cheti? 📄 Una cheti unataka kupata Leseni? 🔄 Unajua kuendesha lakini huna cheti wala leseni na unataka refresh upate cheti? 🛣️ Una nyaraka zote muhimu lakini unahitaji kujifua zaidi barabarani? ✅ Una Leseni bila cheti na unataka renew? 🌍 Tupo mikoa yote Tanzania hadi vijijini! 📞 Tupigie sasa: 0769 763 285
Social Plugin