MASKINI MTOTO HUYU AFARIKI BAADA YA KUKANYAGWA NA GARI LA MAMA YAKE

Mtoto mwenye umri wa miaka sita amefariki baada ya kukanyagwa na gari la mamake.
Bolutito Shodipe mwenye umri wa miaka sita aligongwa na mamake aliyekuwa anajaribu kuegesha gari lake nje ya kituo cha treni cha Hounslow West Tube nyakati za asubuhi Jumatano wiki hii.
Juhudi za kuokoa maisha ya Bolitito katika eneo hilo ziliambulia patupu kwani alisemekana kuaga dunia alipofikishwa hospitalini.
Taarifa kutoka kwa familia ya Bolitito ilisema kuwa wanajaribu kuikubali hali iiliyowakuta kutokana na ajali hiyo mbaya.
Familia hiyo inayoishi eneo la Hayes Magharibi mwa London, iliongeza kusema: "Bolutito alikuwa mtoto wetu wa kwanza na alikuwa nuru kwetu. ''
"alikuwa mrembo, mwenye maadili mema, na mpenzi wa Ballet, na tutamkosa sana.''
Polisi walithibitisha kwamba kifo cha mtoto huyo kilikuwa ajali kwani walifika wote katika kituo cha treni na mamake, ila mtoto aligongwa na kufariki wakati mama akijaribu kuegesha gari lake.

Polisi wanachunguza tukio hilo.
via>>bbc

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
أحدث أقدم