MTOTO ATEKETEA KWA MOTO BAADA YA CHUMBA ALICHOKUWA AMELALA KUUNGUA KWA MOTO

Askari wa jeshi la Polisi akichukua mwili wa marehemu baada ya ajali.



Mtoto mwenye umri wa miaka Mitatu na nusu aliyefahamika kwa jina la Rehema Patrick amefariki dunia baada ya chumba alichokuwa amelala kuteketea kwa moto.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi, amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kuongeza kuwa limetokea leo asaubuhi majira ya saa moja asubuhi huko katika Mtaa na kata ya Ilomba jijini Mbeya.

Amesema chanzo cha moto huo hakijafahamika ambapo mtoto huyo ambaye ni marehemu alikuwa amelala wakati mama yake mzazi aliyefahamika kwa jina la Winfrida Sokon (30), alikuwa ameenda kuchota maji huku naye baba yake akiwa safarini.

Kwa mujibu wa mwenyekiti wa Mtaa, Amiri Kilulu, amesema Mama huyo ni mgeni amehamia jana tu akiwa na watoto wawili ambao ni Tukulamba Mwakyami(4) pamoja na marehemu, lakini huyo mkubwa  ndiye aliyegundua moto huo.

Amesema mtoto huyo baada ya kugundua moto huo alimfuata mama yake alikokuwa akichota maji lakini walipofika walikuta mtoto ameshafariki dunia ambapo majirani walijaribu kuuzima bila mafanikio.

Jeshi la polisi lilifika eneo la tukio na kuondoka na marehemu kwa ajili ya uchunguzi zaidi huku majirani nao wakichangishana fedha kwa ajili ya kusaidia mazishi kutokana na ugeni wa mwanamke huyo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
أحدث أقدم