TAZAMA HAPA TUKIO LA MAADHIMISHO YA MIAKA 20 YA KANISA LA AICT DAYOSISI YA SHINYANGA NA HARAMBEE YA UJENZI WA SHULE YA BISHOP NKOLA

Waumini pamoja na watu wenye mapenzi mema wakiwemo viongozi wa serikali,vyama vya siasa waliohudhuria shereheza maadhimisho ya miaka 20 tangu kuanzishwa kwa dayosisi ya Shinyanga kwa kanisa la AICT,sherehe hizo pia zilienda sambamba na harambee ya kuchangia ujenzi wa shule ya sekondari maarufu kwa jina la Bishop Nkola
Masanja Mkandamizaji akitoa burudani na wacheza shoo wake

Waumini wakifuatilia burudani kutoka kwa waimbaji mbalimbali wa nyimbo za injili kama vile AIC Shinyanga,AIC Kambarage,AKC kwaya,Masanja Mkandamizaji pamoja na CVC Chang’ombe vijana kwaya kutoka jijini Dar es salaam
Chang’ombe vijana kwaya wanafanya mambo ndani ya uwanja wa kambarage mjini Shinyanga
Mgeni rasmi Mbunge wa jimbo la Sengerema mheshimiwa Willium Ngeleja akizungumza uwanjani hapo ambapo aliwataka wananchi kuepuka manabii wa uongo ili kuhakikisha kuwa amani ya nchi inaendelea kuwepo
Askofu mkuu wa kanisa la AICT dayosisi ya Shinyanga Dk John Kanoni Nkola akihubiri katika kilele cha maadhimisho ya miaka ya 20 tangu kuanzishwa kwa kanisa hilo,maadhimisho hayo yamefanyika jana katika uwanja wa CCM Kambarage mjini Shinyanga,ambapo pia kulifanyika harambee ya ujenzi wa shule ya sekondari ya Bishop Nkola inayomilikiwa na kanisa hilo
Kulia ni mkuu wa wilaya ya Shinyanga ndugu Anna Rose Nyamubi akiwa na (Prince Mobutu)na mtoto wa Mobutu Seseseko ambaye pia alihudhuria maadhimisho hayo na kuchangia Euro 2000 pamoja na makontena mawili,moja la nondo jingine la saruji kwa ajili ya ujenzi wa shule ya Bishop Nkola.Mkuu wa wilaya aliuambia umati wa watu waliohudhuria kuwa shule ya Bishop Nkola ni miongoni mwa shule zinazofanya vizuri mkoani Shinyanga.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
أحدث أقدم