ZAWA WATEMBELEA DUWASA

 


Na Mwandishi Wetu, Dodoma 

Watumishi kutoka Mamlaka ya Maji Zanzibar (ZAWA) wametembelea Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dodoma (DUWASA) kwa lengo la kubadilishana uzoefu wa namna ya upatikanaji maji chini ya ardhi.

Wageni hao wametembelea chanzo cha maji cha Nzuguni na kujionea kazi za uchimbaji wa visima zinazoendelea katika eneo hilo.

Jiji la Dodoma linahudumiwa na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dodoma (DUWASA) ambapo sehemu kubwa ya huduma ya maji inapatikana kutokana na visima kama ilivyo upande wa Zanzibar ambao pia sehemu kubwa ya huduma ya maji inapatikana kutokana na visima.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
أحدث أقدم