NAIBU WAZIRI DKT. MOLLEL AANZA ZIARA MKOANI TANGA




Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel leo tarehe 19/10/2023 amewasili Mkoani Tanga na kupokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Waziri Kindamba kwa ajili ya ziara ya kikazi ya siku moja katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo .

Aidha, katika ziara hiyo Dkt.Mollel ameongozana na watalamu mbalimbali kutoka Wizara ya Afya.

Dkt. Mollel atatembelea Hospitali ta Rufaa Bombo kukagua hali ya utoaji huduma na kisha kufanya kikao na watumishi wote wa Hospitali hiyo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
أحدث أقدم