RAIS WA KAMPUNI YA MAFUTA YA SHELL TANZANIA ATEMBELEA BANDA LA TPDC SABASABA

Rais wa Kampuni ya Mafuta ya Shell Tanzania Bw. Jared Kuehl akisaini kitabu cha wageni wakati alipotembelea banda la Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) Julai 6,2023 katika Maonesho ya 47 ya Biashara ya Kimataifa Dar es Salaam yanayoendelea kwenye Viwanja vya Sabsaba Jijini Dar es Salaam.

************

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

RAIS wa Kampuni ya Mafuta ya Shell Tanzania Bw. Jared Kuehl ametembelea banda la Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) katika Maonesho ya 47 ya Biashara ya Kimataifa Dar es Salaam yanayoendelea kwenye Viwanja vya Sabsaba Jijini Dar es Salaam.

TPDC wamekuwa wakishiriki Maonesho hayo mara kwa mara ambapo wanatoa elimu kwa wananchi ambao wanatambelea banda lao ikiwemo kuwaoneha na kuwaelezea miradi mbalimbali inayoendelea kwenye Shirika hilo ikiwemo mradi wa LNG.

TPDC inawakaribisha wadau mbalimbali kuweza kuona na kujifunza Visikuku ambavyo vinasaidia kujua umri wa mwamba na mazingira ambapo mwamba ulitengenezwa baharini au nchi kavu katika uzalishaji wa mafuta na gesi.
Rais wa Kampuni ya Mafuta ya Shell Tanzania Bw. Jared Kuehl akitumia hadubini kutazama visikuku vidogo vidogo vinavyopatikana kwenye miamba wakati alipotembelea banda la Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) Julai 6,2023 katika Maonesho ya 47 ya Biashara ya Kimataifa Dar es Salaam yanayoendelea kwenye Viwanja vya Sabsaba Jijini Dar es Salaam.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
أحدث أقدم