KWA MKAPA HATOKI MTU, SIMBA SC YAONDOKA NA POINTI TATU MBELE YA VIPERS



WAWAKILISHI Katika Michuano ya Klabu Bingwa Afrika timu ya Simba SC imejiweka katika mazingira mazuri ya kutinga Robo Fainali ya Michuano hiyo baada ya kuichpa bao 1-0 Vipers Mchezo wa Kundi C uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. 

Wenyeji walipata bao la kwanza dakika ya 45 likifungwa na Clatous Chama akimalizia pasi ya Moses Phiri na kuipeleka Simba mapumziko ikiwa mbele kwa bao 1-0 dhidi ya Vipers. 

Kwa ushindi huo Simba imefikisha Pointi 6 katika nafasi ya pili na kujiweka nafasi nzuri ya kutinga robo baada ya wapinzani wao wa karibu Timu ya Horoya kupoteza mchezo wake dhidi ya Vinara Raja Casablanca wenyeji Pointi 12,Horoya inashika nafasi ya tatu wakiwa na Pointi 4 huku Vipers ikishika mkia wakiwa na Pointi 1. 

Sasa Simba ili iweze kutinga Robo Fainali inahitaji kupata ushindi katika mchezo wake dhidi ya Horoya Mchezo utakaopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa Machi 17 au 18 mwaka huu.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments