PROF. PALAMAGAMBA KABUDI 'AUTAKA UBUNGE' KILOSA


Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa Prof. Palamagamba Kabudi amesema yupo tayari kuwatumikia wananchi wa jimbo la Kilosa iwapo watamhitaji kwenda kufanya hivyo.


Kabudi ameonyesha nia hiyo leo tarehe 29 Juni 2020 wilayani Kilosa, wakati akihutubia katika hafla ya uwekaji jiwe la msingi ujenzi wa mahandaki manne yenye urefu wa kilomita 2.7 ya reli ya kisasa kutoka Morogoro hadi Makutupora.

Licha ya kwamba hakutaja hadharani nia ya kugombea ubunge Kilosa, Profesa Kabudi amesema, kama atapata kibali kutoka kwa Mungu, hatakataa kuwa mtumishi wa wananchi wa Kilosa.


“Mimi ni kijana wenu, mzaliwa wa hapa na niwaambie kuwa mkinihitaji kuwatumikia niko tayari” amesema Kabudi.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
أحدث أقدم