Snura Akubali Yaishe!! Awaomba Radhi Watanzania Kwa CHURA Yake,Atua BASATA na Kujisajili


Mwimbaji wa muziki wa Mduara nchini Snura Mushi ameomba radhi kwa umma wa Watanzania kwa kosa la kutengeneza, kuzindua na kuweka mitandaoni video ya udhalilishaji wa mwanamke na isiyozingatia maadili ya Kitanzania ya muziki unaoitwa "Chura".

Akizungumza na vyombo vya habari leo Snura amesema wakati wa utayarishaji wa video hiyo mvua ilinyesha hivyo madansa walilowana.

"Baada ya kuona wamelowa ilibidi tusitishe kupeleka katika televisheni na kuiacha you tube, Snura hajafungiwa bali video yangu ilisitishwa na mimi nilizuiwa kujihusisha na sanaa mpaka nijisajili," amesema Snura.

Meneja wa mwanamuziki huyo Hemedi Kavu amesema tayari walishakwenda Basata tangu jana kuomba usajili, leo wamepatiwa cheti cha usajili.


"Tumeshajisajili Basata, pia tayari tumeshaitoa video hiyo kwenye mtandao wa YouTube, tumeshalitekeleza na akaunti ya wimbo huo imeshafutwa na tunatarajia kuifanya video hiyo upya," amesema Hemedi Kavu.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527