Bunge Latolea Ufafanuzi Madai ya Kitwanga Kujibu Swali Bungeni Huku Akiwa Amelewa


BUNGE limekanusha taarifa inayosambazwa katika mitandao ya kijamii na watu wanaodaiwa kuwa ni madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza.


Taarifa hiyo inadai kuwa video iliyomuonesha aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga akijibu swali bungeni Mei 20 mwaka huu, ilihaririwa na kusambazwa na maafisa wa Bunge.


Kitengo cha Habari, Elimu na Mawasiliano cha Bunge kilitoa taarifa ya ufafanuzi kuhusu madai ya kuhaririwa kwa video hiyo, mjini Dodoma jana.


Taarifa hiyo ilieleza kuwa taarifa hizo, si za kweli na zina lengo la kuupotosha umma, kwani ukweli ni kwamba kipindi cha maswali na majibu bungeni, hurushwa moja kwa moja na hupatikana kupitia vituo vyote vya televisheni, vinavyopokea matangazo ya bunge.

Ilisema matangazo hayo, yanaweza pia kurekodiwa na mtu yeyote mwenye uwezo huo popote alipo, kadri anavyoweza kuyapokea matangazo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527