ANGALIA PICHA 100 GHARIKA LA UKAWA UWANJA WA JANGWANI JIJINI DAR ES SALAAM KWENYE UZINDUZI WA KAMPENI ZA UCHAGUZI



Mgombea urais wa vyama vinavyounda katiba ya wananchi UKAWA Mh.Edward Lowasa ameongoza maelfu ya wananchi kuzinduzi rasmi kampeni za vyama hivyo katika uwanja wa jangwani huku akiwataka wataanzania kuhakikisha wanapokea mabadiliko kwa amani kwani kwa sasa hayakwepeki.

Akizungumza na maefu ya wananchi katika uzinduzi huo Mh.Lowasa ambaye amesema akichaguliwa kuwa raisi atahakikisha sekta zote ambazo zimezorota kutokana na kukosa usimamizi ikiwemo Elimu,Kilimo,na sekta ya usafirishaji ukiwemo wa reli na Anga.



Baadhi ya mawaziri waliokihama chama cha mapinduzi akiwemo Mh.Fredrik Sumaye na Laurence Masha ambao pamoja na kumpongeza Mh.Lowasa kwa kuongeza mabadiliko wamesema waliyatamani siku nyingi lakini alishindwa kwa sababu ya mfumo ulioandaliwa kwa makusudi ya kuwatia hofu na kuwatisha huku wakielezea baadhi ya maovu yanayofanyika chini ya serikali ya CCM.

Kwa upande wake mgombea mwenza Mh.Duni Haji amesema maelfu ya wananchi na viongozi wanaendelea kuunga mkono mabadiliko ni ishara ya kutosha kuonyesha kuwa wamechoshwa na uonevu na mabavu ya serikali ya CCM.

Ukafika wakati wa viongozi mbalimbali wa UKAWA wakiongozwa na Mwenyekiti wa CHADEMA Mh.Fereeman Mbowe ambao wamesema dalili ya kwanza ya kuonyesha kuwa viongozi wa CCM hawathamini wananchi ni kujifanya maskini huku wakificha utajiri wao.


ANGALIA PICHA HAPA CHINI

































































Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
أحدث أقدم