SHEREHE ZA MEI MOSI 2015 KUFANYIKA KISHAPU MKOA WA SHINYANGA



Maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani(Mei Mosi) katika mkoa wa Shinyanga yatafanyika Kesho katika uwanja wa  Uhuru uliopo katika mgodi wa Mwadui wilayani Kishapu.

Mwenyekiti wa Vyama  Huru vya Wafanyakazi –TUCTA mkoa wa Shinyanga Fue Mrindoko(Pichani) amesema sherehe hizo zitaanza saa moja asubuhi kwa maandamano  kutoka jengo la Maendeleo vilivyopo katika mgodi wa Mwadui kuelekea kwenye uwanja wa Uhuru uliopo katika mgodi huo.

Mrindoko amesema mgeni rasmi katika sherehe hizo za Mei Mosi zitakazofanyika kesho Ijumaa anatarajiwa kuwa mkuu wa mkoa wa Shinyanga Ally Nassoro Rufunga.

Amewataka wananchi kujitokeza mapema na kwa wingi katika sherehe hizo ambazo zitahudhuriwa na makundi mbali ya wafanya kazi wa serikali,mashirika ya Umma na Taasisi binafsi.

Mrindoko amesema katika sherehe hizo pia kutakuwa na burudani mbalimbali ikiwemo mashindano ya mbio za baiskeli,ngoma,bendi na kuvuta kamba.

Amesema kauli mbiu ya Maadhimisho hayo nchini Tanzania mwaka huu ni “Mfanyakazi Jiandikishe Kura Yako Ina Thamani Kwa Maendeleo Yako”.
Na Kadama Malunde-Malunde1 blog


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
أحدث أقدم