Mchungaji maarufu Afrika Kusini Sthembiso Zondo
ambae huwa anatoa mahubiri yake kwa njia ya Redio nchini humo, ratiba
ya kurushwa kwa mahubiri yake imesimamishwa kurushwa hewani baada ya
kuvuja video inayomuonyesha akizungumza kwenye simu huku akiwa hajavaa
nguo yoyote.
Shirika la utangazaji la Afrika Kusini (SABC) limetoa
amri ya kusimamishwa kwa Kipindi cha mchungaji huyo hadi
itakapotangazwa tena, maamuzi yaliyotolewa baada ya video inayomuonyesha
Mchungaji Zondo
akiwa hajavaa nguo iliyowekwa kwenye mitandao, video hiyo inaonyesha
kuwa ilirekodiwa na mwanamke aliyekuwa amevaa skirt ya pink lakini
hakuweza kutambulika.
Taarifa zinasema kuwa Zondo aliomba
radhi kutokana na kuvuja kwa video hiyo, japo kulikuwa na mvutano pia
wengine wakilaumu aliyevujisha video hiyo huku wengine wakimfata
mchungaji huyo ajieleze kuhusu video hiyo.