YANGA SC YASOGELEA ROBO FAINALI CAFCC, YAINYUKA REAL BAMAKO 2-0


NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

KLABU ya Yanga imefanikiwa kuondoka na alama tatu baada ya kuichapa timu ya Real Bamako kwa mabao 2-0, katika mchezo ambao ulipigwa kwenye dimba la Benjamini Mkapa Jijini Dar es Salaam.

Yanga Sc ilianza kupata bao la kwanza kupitia kwa mshambuliaji wao raia wa DR Congo Fiston Kalala Mayele dakika nane ya mchezo na kuwapeleka Yanga kipindi cha kwanza wakiwa mbele kwa bao 1-0.

Kipindi cha pili Real Bamako walirudi kwa kasi kwani waliengeneza nafasi nyingi pasipo kuzitumia nafasi hizo ndipo Yanga Sc ikafanya mabadiliko ya wachezaji wake, mabadiliko ambayo yalizaa matunda kwani alitoka Tuisila Kisinda na kuingia Jesus Moloko ambaye aliweza kupachika bao la pili na kufanya matokeo kuwa 2-0

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments