YANGA SC KAMA KAWAIDA!! YAIDUNGUA KMKM MAPINDUZI CUP


Na Bolgas Odilo_Mzalendo blog

VINARA wa Ligi Kuu Tanzania bara timu ya Yanga SC imeanza vyema katika Michuano ya Kombe la Mapinduzi CUP 2023 baada ya kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya KMKM mchezo uliopigwa uwanja wa Amani mjini Zanzibar.

Yanga wamepata bao katika dakika za lala salama 90+5 likifungwa na Dickinson Ambundo

Kwa ushindi huo Yanga wanahitaji ushindi dhidi ya Singida Big Stars ili kutinga hatua ya nusu fainali.

Singida Big Stars wanaongoza Kundi wakiwa na Pointi 3 sawa na Yanga ila wakiwa na uwiano wa kufunga mabao.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments