MKE WA PASTA ACHAPANA MAKONDE NA MWANAMKE MWENZAKE LIVE KANISANI


Video moja inasambaa kwenye mtandao wa kijamii ikiwaonyesha wanawake wawili wakipigana kanisani katika eneo la Umuahia, jimbo la Abia nchini Nigeria.

Kulingana na Sunday Ogirima, ambaye alichapisha video hiyo kwenye mtandao wa Facebook, kati ya wanawake hao mmoja ni mke wa pasta na muumini wa kanisa hilo. 

Ogirima ambaye anaonekana kuwa mwandishi wa habari, alisema hawezi kunyamazia kitendo hicho kwa sababu ni cha aibu na ndio maana alianika video hiyo mtandaoni.

Katika video hiyo, mwanamke aliyevalia rinda la blu ndiye mke wa pasta Akaa na anayepokezwa kichapo ni binti ya shemasi wa Kanisa la AG Worship Center.

 Ogirima alifichua kuwa sababu za wawili hao kupigana kanisani ni kwamba Bi Akaa alikuwa amepanga njama na kundi la TAG kunyakuwa kanisa hilo kimabavu lakini mume wake alikataa kushirikiana naye.

Kutokana na kuhofia, shemasi na binti yake walikwenda kufunga kanisa hilo ili kumzuia Bi Akaa kuuza kanisa hilo kwa TAG.

 Bi Akaa aliwakaripia shemasi na bintiye kwa kumzuia kuuza kanisa hilo kwa TAG na kutaka kusalia katika kundi la TST.

 Kisha baada ya kurushiana maneno, mke wa pasta alianza vita na kumtupa chini binti ya shemasi.

Via Tuko news

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments