JINSI TGNP ILIVYOADHIMISHA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA...GEMMA ATAKA KILA MMOJA ALINDE MTOTO

Mwenyekiti wa bodi ya Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) Gemma Akilimali leo Jijini Dar es Salaam akizungumza na wananchi wakati wa Maadhimisho ya siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia ambayo hufanyika kuanzia Novemba 25 hadi Desemba 10 kila Mwaka ambapo amesema ukatili unaofanyika kwenye jamii na ndani kwenye familia ndio unaowadhuru watoto na wanawake ndio unaowanyima haki zao za Msingi.


Amesema kumekuwa na taaarifa za kingono kwenye sekta ya usafiri hasa kwenye magari ya watoto kwa hiyo usalama wa watoto upo hatarini sana hivyo kila mtu awe mstari wa mbele kupinga ukatili wa kijinsi dhidi ya watoto na wanawake.


"Ni jukumu letu Kila mmoja katika jamii ajisikie kuwajibika kumlinda mtoto ili afurahie utoto wake, ujana wake pamoja na kufurahia uzee wake", amesema Gemma.


Akizungumzia kuhusu ufuatiliaji wa sheria ya Ngono amesema kuwa watafuatilia sheria ya rushwa ya ngono, ambayo inakaribia kwenda kujadiliwa bungeni ambayo ina kipengele cha sheria Rushwa ya ngono ni sawa na uhujumu uchumi.


Amesema kuwa Takwimu za Jeshi la Polisi za Januari hadi Desemba 2021 zinaonesha kulikuwa na kesi 5899 za ubakaji, matukio ya ubakaji 1677 na Matukio ya mimba za utotoni 1114 .


Pia amesema kuwa jamii sijionee aibu kukemea matendo ya ukatili wa kijinsia kwani yamefika hadi ngazi ya Familia.


Kwa upande wake Makamu Mkurugenzi wa Shirika la Builders of Future Africa Brenda Mgallah amesema kuwa ukatili ni jambo la kukemewa katika jamii hivyo kila mmoja awe mstari wa mbele kupinga ukatili wa kijinsia.


Naye Mwakilishi wa Serikali ya Mtaa wa Mabibo, amesema kuwa wanashirikiana na TGNP, viongozi wa dini kutoa elimu makanisani na misikitini katika kupinga ukatili wa kijinsia kuanzia ngazi ya mtaa na familia na tayari wameanzisha mabaraza la kata kwa ajili ya kusimamia na kupinga ukatili ya kijinsia maeneo yote yanayoizunguka jamii.


Kauli mbiu ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia Kila uhai una thamani, tokomeza Mauaji ya wanawake na watoto.


Ukatili dhidi ya watoto umekuwa ni sehemu ya maisha ya watoto wengi nchini ambapo asilimia nane ya wanawake na watoto wenye umri wa Miaka 15 hadi wanapata ukatili wa Kingono na wanaofanya ukatili huo ni ndugu wa karibu.
Mwenyekiti wa bodi ya Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) Gemma Akilimali akizungumza na vituo vya Taarifa na Maarifa, viongozi mbalimbali pamoja na wananchi kuhusu taswira halisi ya namna walivyoweza kukabiliana na ukatili wa kijinsia wakati alipokuwa anafanya ufunguzi wa kilele cha maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia ni kampeni ya kimataifa ya kupinga ukatili wa kijinsia yaliyofanyika katika viwanja vya ofisi ya hiyo Leo jijini Dar es Salaam.
Mjumbe wa Bodi ya TGNP Subira Kibiga akimkaribisha mgeni rasmi kwa ajili ya kufungua maadhimisho ya kilele cha siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia ni kampeni ya kimataifa yaliyofanyika katika viwanja vya ofisi ya TGNP jijini Dar es Salaam.
Makamu Mkurugenzi wa Shirika la Builders of Future Africa Brenda Mgallah akizungumza namna wanavyoshirikiana na Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) katika kutoa Elimu kwa jamii kufungua maadhimisho ya kilele cha siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia ni kampeni ya kimataifa yaliyofanyika katika viwanja vya ofisi ya TGNP jijini Dar es Salaam yaliyoanza Novemba 25 Hadi Desemba 10 mwaka 2022.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Binti Makini Janeth Johnakizungumza kuhusu namna wanavyitoa elimu hasa kwa watoto wa kike waliopo mashuleni namna ya kujitambua na kupambana na masuala ya ukatili wa kijinsia kufungua maadhimisho ya kilele cha siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia ni kampeni ya kimataifa yaliyofanyika katika viwanja vya ofisi ya TGNP jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wajumbe mbalimbali wakichangia mada kwenye maadhimisho ya kilele cha siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia ni kampeni ya kimataifa yaliyofanyika katika viwanja vya ofisi ya TGNP jijini Dar es Salaam yaliyoanza Novemba 25 Hadi Desemba 10 mwaka 2022.
Baadhi ya viongozi kutoka Serikalini, mashirika, vituo vya Taarifa na Maarifa pamoja na Wananchi mbalimbali wakiwa kwenye maadhimisho ya kilele cha siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia ni kampeni ya kimataifa yaliyofanyika katika viwanja vya ofisi ya TGNP jijini Dar es Salaam yaliyoanza Novemba 25 Hadi Desemba 10 mwaka 2022.
Mwenyekiti wa Bodi ya Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) Gemma Akilimali akiwa kwenye picha za pamoja na Makundi mbalimbali kama vile viongozi kutoka Serikalini, Mashirika na Taasisi, vituo vya Taarifa na Maarifa pamoja na Wananchi mbalimbali wakiwa wakati wa maadhimisho ya kilele cha siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia ni kampeni ya kimataifa yaliyofanyika katika viwanja vya ofisi ya TGNP jijini Dar es Salaam yaliyoanza Novemba 25 Hadi Desemba 10 mwaka 2022.
Mwenyekiti wa Bodi ya Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) Gemma Akilimali akiwasili kwenye maadhimisho ya kilele cha siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia ni kampeni ya kimataifa yaliyofanyika katika viwanja vya ofisi ya TGNP jijini Dar es Salaam yaliyoanza Novemba 25 Hadi Desemba 10 mwaka 2022.

Maandamano yakiendelea
Burudani zikiendelea

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments