JUVENTUS YAKUBALI KUMUUZA BEKI WAKE WA KIMATAIFA MATTHIS De LIGT KWENDA BAYERN MUNICH





Beki wa kimataifa wa Uholanzi, Matthijs de Ligt ambaye amekubali kujiunga Bayern Munich akitokea Juventus

KLABU ya Juventus ya Italia imekubali kumuuza Beki wake wa kati, Matthijs de Ligt (22) kwenda kwa mabingwa wa Ujerumani Bayern Munich kwa ada ya Paundi Milioni 68 (Tsh. 186,320,000,000)

Taarifa kutoka Ujerumani zinaeleza kuwa beki huyo wa kimataifa wa Uholanzi atasaini mkataba wa miaka mitano na Bayern mara baada ya kukamilisha vipimo vya afya anavyotarajia kufanya leo katika jiji la Munich.

De Ligt anaondoka Juventus akiwa amekaa kwa misimu mitatu, akicheza mechi 177 na kufunga magoli nane. pia, alishinda taji la Serie A katika msimu wa 2019/20.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments