KIJANA AJINYONGA KWENYE GOLI LA UWANJA WA MPIRA AKIWA NA NGUO YA NDANI YA MWANAMKE

Picha ya nguo ya ndani ya mwanamke haihusiani na habari hapa chini

Na Amiri Kilagalila, Njombe
Tyson Kilasi (32) mkazi wa Kijiji cha Mawindi halmashauri ya wilaya ya Wanging’ombe mkoani Njombe, amekutwa amefariki kwa kujinyonga kwenye goli la uwanja wa mpira wa miguu wa uliopo kijijini hapo huku pembeni akiwa ameacha nguo ya ndani ya kike.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Mawindi, Kata ya Igima bwana Elias Mwinami amethitibitisha kutokea kifo cha kijana huyo kilichotokea usiku wa kuamkia leo Januari 18, 2022.

Mwinami amesema chanzo cha kifo cha kijana huyo bado hakijafahamika ambapo eneo ambalo mwili wa kijana huyo wameukuta ni eneo la goli la mpira wa miguu na wamekuta nguo ya ndani ya mwanamke.

“Tumemkuta asubuhi ananing’inia kwenye goli lakini chanzo bado hakijafahamika na kimsingi tunalaani kitendo hiki ifike mahali tuelimike na hivi karibuni tu polisi walikuja kutoa elimu kwa kweli wananchi waache kujichukulia sheria mkononi,” alisema Mwinami.

Akizungumza kwa njia ya simu Diwani wa kata ya Igima bi. Paulina Samata Mwinami amesema kata ya Igima inahitaji juhudi za pamoja kuelimisha wananchi juu ya kuacha kujichukulia sheria mkononi na kwamba tukio hilo ni la pili kutokea kwenye kata hiyo.

Bi. Mwinami amesema wiki moja imepita mwanaume mmoja na mwanamke mmoja walikutwa wameuawa katika misitu ya kampuni ya Tanwat ambao walitambulika kuwa ni wakazi wa kata ya Igima mmoja wa kijiji cha Mawindi na mwingine mkazi wa kijiji cha Mhaji ambao uchunguzi wa polisi bado unaendelea.

“Nilivyojaribu kuuliza kama jana ulitokea ugomvi wamesema hawaelewi kwa kweli ninajiskia vibaya mno kwasababu watu sasa wanajichukulia sheria mkononi.Niombe wananchi kama wanakuwa na kitu ni vema wawe wanakitoa kuliko kuchukua uamuzi wa kujiua,” alisema Paulina Samata.

Baadhi ya wananchi na majirani wa marehemu huyo wamesema serikali iongeze kasi ya kuelimisha wananchi kupitia mikutano ili kupunguza matukio ya vifo katika kata hiyo na kwamba migogoro katika familia, ardhi na uhusiano wa kimapenzi ndiyo inayohisiwa kuwa chanzo cha matukio hayo.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

1/Post a Comment/Comments


  1. UCHAWI HATARI ZAIDI KULIKO UCHAWI WOWOTE WA MAPENZI:

    Katika masuala ambayo uchawi una ishi na kutawala basi ni suala la mapenzi.
    Asilimia kubwa ya watu wanao enda kwa waganga, huenda huko kwa sababu ya mapenzi au kwa sababu ya mambo yanayo sababishwa na mapenzi.
    Uchawi wa mapenzi upo wa aina nyingi sana. Nikisema nianze kutaja na kuelezea kwa kila aina ya uchawi na ulozi katika mapenzi hapa, sitamaliza kwa sababu upo uchawi wa aina nyingi sana.
    Nitataja na kuelezea kwa ufupi sana, aina chache za uchawi katika mapenzi, halafu nitaelezea aina moja ya uchawi wa mapenzi ambao ni uchawi hatari na wenye nguvu sana.

    KUMSHIKA MWANAUME KATIKA MAPENZI:
    Kumshika mwanaume katika mapenzi, wachawi huchukua njiwa wawili jike dume walio zaliwa kiota kimoja pamoja na kiota chawe, kisha njiwa hao huchinjwa , hupasuluwa na mioyo yao hunyofolewa, huchemshwa kwenye mafuta ya mti mmoja unapatikana porini, halafu husagwa hadi kuwa unga unga. Baada ya hapo huchukua njugu mawe nyeusi moja, huchanganya na mti unaitwa mlama, pamoja na miti mingine mitatu ya porini, kisha husagwa pamoja na ile mizoga ya njiwa.
    Vyote hivi kwa pamoja, huchanganywa na vizimba vitatu vya ndumba za kichawi, halafu mwanaume huwekewa kwenye chakula, basi mwanaume huyo atakuwa hasemi chochote kwa mwanamke huyo.Mwanamke atakuwa mama ake atakuwa baba ake. Ni uchawi mbaya sana huu.

    KUMFANYA MWANAUME ASIENDE NJE YA NDOA :
    Kumfanya mwanaume asiende nje ya ndoa, wachawi huchukua kamba ya mbuzi, moyo wa kondoo, mti unaitwa INAMA NIKUCHUME ( Mti huu unapatikana Kigoma tu, na watu wa kigoma ndio huuita jina hilo), mti unaitwa Inyazya kisha vinasagwa kwa pamoja halafu vinachanganywa na nta ya nyuki, kisha wanatafuta kucha, au nywele, au ndevu, au uzi wa nguo yake yoyote, halafu vinakaangwa kwa chumvi ya mawe pamoja na vizimba vya zote nilizo zitaja hapo juu, kisha vinafungwa kwenye kitambaa chekundu, halafu vinafukiwa mlangoni au kwenye mti wowote. Basi mwanaume huyu hawezi kwenda nje ya ndoa yake.

    MWANAUME AKUONE WEWE TU KILA ANAPOKUWA NA MWANAMKE MWINGINE : Wachawi huchukua maji ambayo mwanamke ametumia kunawa uso wake kisha huchanganya na ndumba 13 za kichawi pamoja na vizimba vyake kisha kutengeneza ndumba itakayo mfanya mume wa mwanamke huyo kuwa anaumuona mke wake wakati wote na pia kuwa anaona kama anatokewa na mke wake kila anapo kuwa na michepuko.

    KUMFANYA MUME AKUPE MSHAHARA WAKE WOTE AU PESA ZAKE ZOTE KILA AKIZIPATA: Uchawi huu umewalostisha wanaume wengi sana. Hapa mchawi anacho chukua manii za mwanaume aliye mkusudia, ana changanya pamoja na baadhi ya vitu alivyo pewa na mwanaume huyo, halafu vinaenda kutengenezwa kichawi kwa kutumia ndumba za kichawi, basi mwanaume huyo atakuwa kila akipata mshahara wake anapeleka zote kwa mwanamke huyo. Asipojistukia mapema, anaweza uza kila kilicho chake.

    KUMVUTA MPENZI : Ipo miti mitatu inapatikana porini, miti hutumika kumuita kichawi mwanamke au mwanaume aliye kusudiwa.

    SIKU NYINGINE NITAELEZEA KWA UREFU SANA KUHUSU UCHAWI MBALIMBALI UNAO TUMIKA KATIKA MAPENZI.

    Acha kupoteza pesa pasipo na matumaini wala mafanikio kwa watu wa laghai, kwa tiba mujarabu za kissunah na kisomo cha kisheria(Ruqyah) usisite kuwasiliana nami mnajimu na tabibu wa tiba mbadala na maradhi sugu sheikh Mohamed kwa mawasiliano 👇🏿

    +255 715 277 200 Whatspp/Call

    ReplyDelete

Post a Comment