TANGA UWASA YAELEZA SABABU YA MGAWO WA MAJI JIJINI TANGA

 

Kaimu Mkurugenzi wa Tanga Uwasa Mhandisi Rashid Shabani  kulia akizungumza na waandishi wa habari mapema leo wakati akitoa taarifa kwa Umma Juu ya uwepo wa upungufu wa upatikanaji wa Huduma ya Maji Safi kwa Wakazi wa Jiji la Tanga kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Huduma kwa Wateja Tanga Uwasa Rogers 
Kaimu Mkurugenzi wa Tanga Uwasa Mhandisi Rashid Shabani  kulia akizungumza na waandishi wa habari mapema leo wakati akitoa taarifa kwa Umma Juu ya uwepo wa upungufu wa upatikanaji wa Huduma ya Maji Safi kwa Wakazi wa Jiji la Tanga kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Huduma kwa Wateja Tanga Uwasa Rogers Machaku
AFISA Uhusiano wa Tanga Uwasa Dovetha Mayala akisisitiza jambo
Sehemu ya waandishi wa Habari wakifuatilia matukioo mbalimbali kwenye mkutano huo


NA OSCAR ASSENGA, TANGA.

MAMLAKA ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Tanga (Tanga Uwasa) imeeleza sababu za kuanza kwa mgao wa maji katika Jiji la Tanga kwamba inatokanana na kiasi kilichopo cha maji yanayozalishwa kiweze kusambazwa na kupatikana kwa watu wote .

Hivyo kusababisha uwepo kwa upungufu mkubwa wa maji katika maeneo ya Jiji la Tanga lenye wakazi wapatao 316,055 Tangu mwishoni mwa mwezi Septemba 2021.

Mgao huo unatarajiwa kuanza Octoba 9 mwaka huu katika maeneo ya Nguvumali, Kisosora,Mwamboni, Chumbageni, Kwaminchi,Chuda,Gofu,Ngamiani,Central,Bombo,Raskazone,Sahare,Usagara na Makorora.

Maeneo mengine yatakayoathirika na mgao huo ni Duga, Magomeni, Mabawa, Mwakizaro,Msambweni,Donge, Magaoni,TangaSisi,Mwang’ombe,Mwakidila,Mwahako,Masiwani,Mbugani,Machui,Tongoni,Kiwavu,Maere,Kivindani,Mtakuja na Kange Kasera.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Kaimu Mkurugenzi wa Tanga Uwasa Mhandisi Rashid Shabani ambapo alisema hilo linatokana na kwa kuzingatia majira ya mwaka Jijini Tanga ambapo kipindi cha kiangazi huanza mwezi Agosti hadi Novemba kila mwaka.

Alisema ambapo kipindi hicho matumizi ya maji huongezeka na hivyo kujitokeza kwa upungufu wa maji maeneo mengi kutokana na maji yanayozalishwa kutokukudhi mahitaji ya maji kwa watu wote Jijini Tanga kwa kipindi hicho.

“Upungufu huu unatokana na ukomo wa uzalishaji maji wa mtambo wa kusafisha na kutibu maji Mowe kwani uwezo wa kuzalisha na kusambaza maji ni wastani mita za ujazo 30000 kwa siku wakati mahitaji ya maji wakati wa kiangazi yanakadiriwa kufikia wastani wa mita za ujazo 37100 kwa siku.

Alisema mgao huo umezingatia uwepo wa maeneo mengine yenye ofisi za Umma,Vituo vya Afya ,Hospitali pamoja na taasisi za elimu ambako muda mwingi wa mchana huduma ya maji inabidi iwepo.

Hata hivyo Kaimu Mkurugenzi huyo ambaye pia ni Meneja Ufundi wa Tanga Uwasa alisema kufuatia changamoto hiyo Rais Samia Suluhu pamoja na jitihada za Mbunge wa Jimbo la Tanga Ummy Mwalimu na ufuatiliaji makini wa karibu wa Waziri wa Maji Jumaa Aweso.

Alisema jitihada hizo zimeiwezesha Tanga Uwasa kupata fedha kiasi cha Sh.Bilioni 9.8 ili kutekeleza mradi mkubwa unaolenga kuongeza uwezo wa uzalishaji na usambazaji wa maji kutoka mita za ujazo 30,000 hadi 45,000 kwa siku ambapo ujenzi wa mradi huo ulianza mwezi Agosti mwaka huu na unatarajiwa kukamilika mwezi Agosti 2022.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments