WACHIMBAJI WANNE WAFARIKI KWA KUFUKIA NA KIFUSI MGODINI SIMIYU

Wachimbaji wanne katika mgodi wa dhahabu wa Namba Mbili uliopo kijiji cha Ilujamate Wilaya ya Busega Mkoa wa Simiyu wamefariki dunia baada ya kufukiwa na vifusi baada ya kuta za duara kuporomoka kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha.

Tukio hilo limetokea Aprili 12,2021 saa 4:25 usiku katika duara namba 18 na 17 AB na kusababisha vifo vya wachimbaji wanne na mwingine mmoja kujeruhiwa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Simiyu, Richard Abwao amesema aliyejeruhiwa ni Mangu Ngumba (33) mkazi wa Matongo Wilaya ya Bariadi na waliopoteza maisha ni Limbu Kisabo (28) mkazi wa Mwakibuga Wilaya ya Bariadi na Tembo Male (42) mkazi wa Isanga Bariadi.

Wengine ni Benjamini Masaka (51) mkazi wa Katoro Geita na Musa Washa (37) mkazi wa Dutwa Bariadi.

Via Mwananchi

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments