MAHAKAMA YAMWACHIA HURU ALIYEIBA MAHINDI YAKANASA KICHWANI

Mahakama ya Mwanzo Mlandizi mkoani Pwani imemuachia huru, kijana Frank Joseph (23) aliyeiba kiroba cha Mahindi debe 1 na kumnasia kichwani baada ya mlalamikaji kutofika mahakamani hapo mara 3 mfululizo.


Frank ambaye ni mkazi wa Mbezi Dar es salaam, ameachiwa huru na Hakimu Mfawidhi, Nabwike Mbaba wakati shauri hilo lilipoitishwa kwa ajili mlalamikaji (mtendewa) kutoa maelezo ya jinsi alivyoibiwa.

Hakimu Mbaba amesema kuwa kutokana na mlalamikaji (mtendewa) kushindwa kufika mahakamani hapo mara 3 mfululizo kutoa maelezo ya kuibiwa kwake anaifuta kesi huyo.

“Mtendewa ameshindwa kufika mahakamani licha ya kupewa wito mara 3 mfululizo, hivyo naifutilia mbali kesi hii na mshtakiwa kuanzia sasa upo huru,” amesema Hakimu Mbaba.

Awali mshtakiwa alishindwa kufikishwa mahakamani mara 2 mfululizo kutokana na gari la Magereza kuharibika.

Katika kesi hiyo namba 124/2018 Frank anadaiwa kutenda kosa la wizi May 3, 2018 saa 7 usiku maeneo ya Mlandizi ambapo aliiba Mahindi debe 1 likiwa na thamani ya Sh.20, 000 ikiwa mali ya Seve Seleman.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527