KAMANDA MAMBOSASA AZUNGUMZIA MABILIONI YA DK. SHIKA

Kamanda wa polisi kanda maalum ya Dar es salaam Lazaro Mambosasa amesema suala la Dk. shika kuingiza pesa zake Tanzania hana uhakika nalo na mtu kutumiwa hela kihalali si kosa 


Amesema kuwa kama taarifa hizo ni za uongo anaweza kupuuzwa ila endapo kauli yake italeta madhara basi hatua zitachukuliwa.


Mambosasa amezungumza hayo leo pindi alipokuwa anaongea na waandishi wa habari akitoa ripoti za jeshi la polisi kuwashikilia watuhumiwa mbambali kwa kufanya makosa ya unyang’anyi kwa kutumia silaha za moto.


”Mtu kutumiwa hela kama ni halali haziingii kwenye pesa ambazo zinatakatishwa au hela ambazo zinapatikana kwa njia isiyo halali si kosa lakini kama ni muongo tu anajisema basi kuna mawili anaweza kupuuzwa lakini kama kauli zake zitamwaathiri yeyote anaweza kuja kulalamika na jeshi la polisi likachukua hatua” amesema Mambosasa.


Mambosasa amezungumza hayo pindi alipokuwa anajibu swali la mmoja wa waandishi wa habari baada ya kuhoji juu ya uhalali wa pesa za Dk. Luis Shika ambaye hivi karibuni taarifa zimeeleza tayari ameingiza mabilioni yake ya fedha nchini Tanzania.


Siku chache zilizopita Dkt. Louis Shika alivieleza baadhi ya vyombo vya habari nchini juu ya ujio wa fedha zake na baadhi ya vipande vya dhahabu zilizokuwa nje ya nchi kuwa tayari zimewasili nchini kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere (JKNIA) na kupelekwa Benki Kuu ya Tanzania (BOT) kwa ajili ya kuhakikiwa.


Taarifa hizo zilizua mjadala mkubwa mtandaoni ambapo watu walionesha kutokuamini kwa ujio huo wa pesa za Dk. Shika wakidhani ni stori zisizo na ukweli ndani yake.


Hata hivyo Shika alithibitisha ujio wa mali hizo na kuonyesha baadhi ya nyaraka zinazothibitisha umiliki wa mali hizo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527