DAKTARI ABURUZWA MAHAKAMANI KWA KUIBA MOYO WA MAREHEMU


Mkuu wa zamani wa uchunguzi wa chanzo cha vifo nchini Kenya ameshtakiwa kosa la kuiba moyo kutoka kwenye maiti iliyokuwa inafanyiwa upasuaji.

Dkt. Moses Njue alikanusha shitaka hilo aliposomewa mashitaka yake katika Mahakama ya Hakimu Mkuu Nairobi ambapo alikuwa ameshitakiwa yeye na mwanae pamoja msaidizi wake.

Walidaiwa kuiba moyo wa Timothy Mwandi Muumbo wakifanyia mwili wake upasuaji Juni 25, 2015 katika chumba cha kuhifadhia maiti cha 'Lee Funeral Home'.

Hakimu Mkuu Francis Andayi aliagiza watuhumiwa wengine wafike Mahakamani na kujibu mashitaka kabla ya kesi kuanza kusikilizwa Julai 3.

Dkt. Njue alikanusha pia shitaka jingine la kuuharibu moyo ili kuficha ushahidi, akifahamu kwamba ripoti ya uchunguzi wa maiti hiyo ingetumiwa kwenye kesi iliyokuwepo Mahakamani.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527