SERIKALI YATANGAZA NEEMA KWA WATUMISHI WA UMMA

SERIKALI imetangaza neema kwa watumishi wa umma 4,812 baada ya jana kubainisha kuwa kuna fursa za mafunzo 659 zitakazotolewa na Serikali ya China.


Fursa hizo za mafunzo zimejikita kwenye maeneo ya kipaumbele cha taifa yaliyoainishwa katika Mpango wa Taifa wa Miaka Mitano (2016/17-2020/21).


Katika mkutano wake na waandishi wa habari kwenye Ukumbi wa Idara ya Habari na Elimu ya Bunge mjini hapa jana, Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dk. Laurean Ndumbaro, alisema mafunzo yamejikita kwenye uhandisi wa viwanda, mawasiliano na usafirishaji.


Dk. Ndumbaro pia alisema mafunzo hayo yatajikita kwenye kilimo, elimu, afya, biashara na uchumi, Tehama na utawala bora.


Alisema gharama za mafunzo hayo zitagharamiwa na Serikali ya Watu wa China kuanzia usafiri wa ndege kwenda na kurudi, malazi, chakula na ada.


"Serikali, waajiri watatakiwa kuwawezesha watumishi walio chini yao kuomba na kuhudhuria mafunzo hayo kulingana na sheria, kanuni na taratibu za utumishi," alisema Dk. Ndumbaro.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527