Picha : DC MATIRO AFANYA ZIARA KATA YA SOLWA SHINYANGA VIJIJINI KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO


Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro amefanya ziara katika kata ya Solwa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga kukagua miradi ya maendeleo na kusikiliza kero za wananchi.



Matiro alitembelea vijiji vyote vya kata ya Solwa kukagua miradi ya maendeleo na kufanya kazi na wananchi ikiwa ni pamoja na kuwaunga mkono wananchi wa Solwa kwani ni kata inayoongoza kwa wananchi kuchangia katika shughuli za maendeleo.


Akizungumza wakati wa ziara yake hiyo aliyoifanya hivi karibuni,Matiro aliwapongeza wananchi wa Solwa kwani wanashiriki viziri katika shughuli za maendeleo wakiongozwa na diwani wa kata hiyo Mbaraka Awadh

Nimekuwekea picha wakati wa ziara hiyo
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro katikati akipokelewa na viongozi wa kata ya Solwa wakati wa ziara yake katika kata hiyo
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akiwa katika jengo la wodi ya wazazi ya zahanati ya Solwa linayojengwa kwa nguvu za wananchi

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akishiriki ujenzi
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akipanda katika shule mpya ya Msingi Solwa inayojengwa na wananchi
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akipanda mti
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akiruka maji wakati wa ziara yake katika kata ya Solwa
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza na wanafunzi wa shule ya msingi Solwa
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akimbeba mtoto Elisha ambaye ni mlevamu ambapo aliahidi kumtafutia baiskeli baada ya wanafunzi kuomba msaada wa baiskeli kwa mtoto huyo
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akiwa na mtoto Elisha
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza jambo
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akifurahia jambo na wanafunzi
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza katika shule hiyo
Mkuu huyo wa wilaya akitembelea bustani ya mboga ambao ni mradi wa shule na kuwapongeza walimu kwa kufundisha kwa vitendo


Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akiondoka katika shule ya msingi Solwa

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza na wanafunzi wa shule ya sekondari Solwa
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akiwa katika eneo la ujenzi wa mabweni shule ya sekondari Solwa
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akishiriki ujenzi wa mabweni mawili ya wasichana katika shule ya sekondari Solwa 


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527