NANDY AOMBA RADHI KWA VIDEO YAKE YA UCHI MTANDAONI

Video ya msanii Faustina Charles maarufu Nandy inayomuonyesha akiwa faragha na mwanaume leo imezua gumzo mitandaoni ambapo mwenyewe amefunguka.


Nandy amekiri kwamba video hiyo ni ya kweli japo ni ya mwaka 2016 na kuwaomba Watanzania na Serikali msamaha kwa walichokiona.

Akielezea zaidi, amesema video hiyo ilichukuliwa akiwa katika uhusiano na mmoja wa wasanii wa Bongo Fleva (jina tunalihifadhi), ambapo walikubaliana yawe ya siri.

“Sielewi ana maana gani kuitoa video hiyo kwa sasa na kufika kwenye mitandao, kwani ni vitu kama hivi vinafanyika kwa mtu yeyote anayekuwa kwenye mahusiano,” amesema.

“Nimesikitishwa sana na kitendo hicho na ‘ilishutiwa’ kwa mtindo wa ‘Snapchat’ na sijui kwa nini ameamua kuirushia sasa hivi, yaani sielewi nifanye nini.”

“Naomba radhi kwa mashabiki wangu, familia yangu, kanisani kwangu, Serikali kiukweli video imenichafua sana ila adhabu ya maumivu haya ninayoyapata sasa hivi ni kutokana na kumuamini mtu.”

“Sina cha kusema kwani hiki siyo kitu cha kwanza, kwani ni’shakuwa na mahusiano na mtu huko nyuma na akatishia kutoa picha zangu mpaka pale nilipoenda kuripoti polisi.”

Hata hivyo, Nandy amewaasa vijana kuwa waangalifu wanapokuwa katika uhusiamo kwani tukio hilo wengi wamelichukulia kama ‘kick’.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527