MBWA WAUA WATU WATANO MOSHI





 
Watu watano wamefariki dunia wilayani Moshi mkoani Kilimanjaro baada ya kung’atwa na mbwa wenye kichaa.

Daktari bingwa wa magonjwa ya dharura na ajali wa Hospitali ya Rufaa ya KCMC, Dk Francis Sakita amewaambia wanahabari leo Aprili 12,2018  kuwa ugonjwa huo umekuja kwa kasi kubwa ukilinganisha na miaka mingine.

Amesema kwa kipindi cha Januari hadi Machi vimetokea vifo vitano.

"Hii sio hali ya kawaida kutokea idadi kubwa ya watu kufariki dunia kwa kung'atwa na mbwa wenye ugonjwa huu, idadi hii ni kubwa sana na wengi walioathirika ni watu ambao wako Moshi vijijini. Hii inatokana na watu kutozingatia kupeleka mbwa wao kwenye chanjo," amesema Dk Sakita.
Na Janeth Joseph, Mwananchi

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527