HAYA HAPA MAJINA YA WANAJESHI WOTE WALIOPANDISHWA VYEO NA RAIS MAGUFULI

Rais John Magufuli leo amewapandisha vyeo maofisa wa Jeshi la Ulinzi wa Wananchi (JWTZ) akiwamo Meja Jenerali Peter Massao aliyepandishwa kuwa Luteni Jenerali.

Taarifa iliyosomwa na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania, Jenerali Venance Mabeyo leo Aprili 12, Ikulu Jijini Dar es Salaam imeeleza kuwa Meja Jenerali Massao ni Mkuu wa Chuo cha Mafunzo ya Maaofisa Wanafunzi wa Jeshi Monduli (TMA) na kwa uteuzi huo, sasa JWTZ itakuwa na maluteni jenerali wawili.

Wengine waliopandishwa vyeo na Rais Magufuli ni Brigedia Jenerali Henry Kamunde aliyepandishwa na kuwa meja jenerali.

Pia amewapandisha vyeo maofisa 27 wa JWTZ kutoka cheo cha kanali na kuwa brigedia jenerali na ofisa mmoja kutoka luteni kanali na kuwa kanali.

Waliopandishwa vyeo hivyo ni D.D.M Mullugu, J.J Mwaseba, A.S Mwamy, R.K Kapinda, C.D Katenga, Z.S Kiwenge, M.A Mgambo, A.M Alphonce, A.P Mutta, A.V Chakila, M.G Mhagama, V.M Kisiri, C.E Msolla na S.M Mzee.

Wengine ni C.J Ndiege, I.M Mhona, R.C Ng’umbi, S.J Mnkande, A.C Sibuti, M.M Mumanga, I.S Ismail, M.N Mkeremy, G.S Mhidze, M.A Machanga, S.B Gwaya, P.K Simuli na M.E Gaguti.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527