AUNTY LULU AJIPATIA WACHUMBA WATATU CHINA KWA GIA YA MAKALIO

Mtangazaji na muigizaji wa Bongo movie Lulu Semagongo maarufu kama aunty Lulu amewaacha watu wengi midomo wazi baada ya kudai kalio lake kubwa limemsaidia kupata wachumba watatu nchini China.


Kwenye mahojiano na Global Publishers Aunty Lulu alifunguka na kudai kuwa kwenye Safari yake ya kibiashara nchini China hivi karibuni alihudhuria kwenye ukumbi mmoja ambao kulikuwa na msanii ambaye ni Mtanzania ambaye alikuwa anapiga shoo.


Aunty Lulu amedai baada ya muziki kuanza kupigwa alianza kucheza na kukata mauno kiasi ya kwamba wanaume walianza kumtolea macho na usiku huo alipata wachumba watatu ambao wapo tayari kumuoa.


"Kalio langu limenipatia wachumba wa Kichina watatu, sasa baada ya wote kuniambia wanataka kunioa, niliwatajia mahari yangu kuwa ni shilingi milioni 50 na walikubali, lakini niliwapa mtihani mwingine kwamba atakayekuwa wa kwanza kufika Bongo ndiye atakayenioa, hivyo ninasubiri na ndoa yangu itakuwa ya mkataba”.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527