ASKOFU MORAVIAN AWATAKA WATANZANIA KUACHA KULALAMIKA

Askofu Kiongozi wa Moravian Tanzania jimbo la Kusini Magharibi Alinikisa Cheyo, amewaasa Watanzania kuacha kulalamika na badala yake wajikite katika kufanya kazi njema inayompendeza Mungu.


Askofu Cheyo ametoa kauli hiyo katika ibada ya Pasaka iliyofanyika katika Kanisa Moravian Tanzania jimbo la kusini Magharibi ushirika wa Mbeya Mjini.

Askofu amesema ili Watanzania waweze kujiletea maendeleo yenye tija kufikia uchumi wa kati wanapaswa kuachana na mambo ya kisiasaili waweze kufanya shughuli zao za kujiingizia kipato.

Askofu Cheyo pia ametumia fursa hiyo kuwaasa viongozi wake wengine wa dini nchini kutofautisha dini na siasa ili kujenga upendo miongoni mwa Watanzania ikiwa ni pamoja na kudumisha amani ya nchi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527