MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA AWAKALIA KOONI CHADEMA..AWAPA SIKU TANO ZA KUJIELEZA TENA


Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi kwa mara nyingine ametoa siku tano kwa Chadema kujieleza kwa nini asikichukulie hatua kwa kukiuka sheria na kanuni za maadili ya vyama vya siasa.


Katika barua hiyo ya Jaji Mutungi ya Machi mosi, 2018 iliyopokelewa Chadema Machi 2 inatakita chama hicho kikuu cha upinzani nchini, kujieleza kwa nini kilivunja sheria na kanuni hizo Februari 16, 2018.

Barua hiyo ya Jaji Mutungi inatokana na kutoridhishwa na majibu ya barua yake ya Februari 21 aliyokiandikia chama hicho, akikipa siku tano kujieleza kwa nini kilivunja sheria na kanuni hizo.

Akizungumza na Mwananchi Digital leo Machi 4, 2018, mkurugenzi wa itifaki, mawasiliano na mambo ya nje wa Chadema, John Mrema amesema barua hiyo wameipokea jana na kesho wanatarajia kuijibu.


Na Ibrahim Yamola - Mwananchi

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527