COASTAL UNION YAPOKEWA KISHUJAA,WAZIRI UMMY,RC SHIGELLA WAONGOZA MAPOKEZI


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu akiwasalimia wakazi wa Mji wa Pongwe mara baada ya kuwasilia na timu ya Coastal Union ikitokea mkoani Morogoro ambapo iliweza kupanda daraja baada ya kuifunga Mawenzi ya Morogoro mabao 2-0 kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martini Shigella 
Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martini Shigella kulia akizungumza wakati alipoipokea timu ya Coastal Union mara baada ya kupanda daraja kucheza Ligi kuu msimu ujao mapokezi hayo yalifanyika kwenye eneo la Pongwe Jijini Tanga kushoto ni  Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu
Mbunge wa Jimbo la Tanga (CUF) Alhaji Mussa Mbaruku akizungumza katika mapokezi hayo 
Wapenzi wa soka mkoani Tanga pamoja na wananchi wakiwa wamezingira barabara ya Tanga kwenye mikoani eneo la Pongwe wakiilaki timu ya Coastal Union leo
Mbunge wa Jimbo la Tanga (CUF) Alhaji Mussa Mbaruku akizungumza katika mapokezi hayo akizungumza katikani ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martini Shigella 
Mwenyekiti wa timu ya Coastal Union,Steven Mguto katikati akimsikiliza kwa umakini Mwenyekiti wa kamati ya usaji wa klabu hiyo Ahmed Aurora kushoto ni Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu mkoani Tanga(TRFA) Saidi Soud
Mfungaji wa moja ya mabao yaliyoipandisha timu ya Coastal Union Athumani Iddi Chuji akizungumza kwenye mapokezi hayo leo (Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha)

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527