CCM YASITISHA KAMPENI ZAKE LEO ILI KUSHIRIKI MAZISHI YA KINGUNGE

Uongozi wa CCM mkoa wa Dar es Salaam umesitisha kampeni za nje kwa siku moja (leo) kwa ajili ya kushiriki mazishi ya mwanasiasa mkongwe, Kingunge Ngombale Mwiru.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu wa Siasa na Uenezi wa chama hicho, Simon Mwakifwamba imeeleza kuwa wanachama, makada na viongozi watashiriki kikamilifu katika msiba huo, hivyo hakutakuwa na kampeni za nje.

Alisema watazingatia ratiba iliyotolewa na msimamizi wa msiba huo Omary Kimbau, hivyo wanaCCM wafike mapema kwa ajili ya kumpumzisha kwenye makazi ya milele komredi Kingunge.

Mwananchi

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527