JAJI MSTAAFU ROBERT KISANGA AFARIKI DUNIA

Rais wa Chama cha Majaji Wastaafu, Thomas Mihayo akizungumza na MCL Digital leo Jumatano Januari 24,2018 amesema Jaji Kisanga alifariki dunia jana jioni.

Jaji Mihayo amesema Kisanga alifariki dunia akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Regency jijini Dar es Salaam.

Amesema taarifa zaidi zitatolewa baadaye.

Mbali ya shughuli za Mahakama, Jaji Kisanga alikuwa mwenyekiti wa kwanza wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora nchini.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527