ZITTO AWAOMBA WATANZANIA WAICHANGIE ACT- WAZALENDO


Kiongozi wa Chama cha ACT- Wazalendo, Zitto Kabwe amewaomba Watanzania kukichangia Chama hicho ili kiweze kuwafikia na kuwaeleza mambo makuu mawili wakati wa mikutano ya kampeni ya udiwani.

ACT- Wazalendo imesimamisha wagombea 28 kati ya 43 katika uchaguzi mdogo wa udiwani utakaofanyika Novemba 26 ambapo kampeni zake zimeanza Oktoba 29.

“Nachukua fursa hii kuwaomba Watanzania wenye uchungu na nchi yetu kuchangia kampeni zetu. Tunataka kufika kila ya kona ya nchi yetu na wewe ndio utatuwezesha kufika,” amesema Zitto

“Chochote ulicho nacho tunaomba utuchangie kwa kutumia namba hizi hapa. Tigo pesa 0713957977 na M-Pesa 0744959112, Asante Sana,” ameongeza

Zitto ambaye ni Mbunge wa Kigoma Mjini Chama hicho kitatumia kampeni hizo kuwaeleza Watanzania mambo makuu mawili ambayo ameyataja kuwa ni ukiukwaji mkubwa wa haki za wananchi na hali ngumu ya maisha ya wananchi.

“Lengo kubwa ni kuwaamsha Watanzania kukataa ubinywaji wa haki za binaadamu na kutaka mabadiliko ya sera za uchumi ili kuongeza ajira na kuondoa umasikini,” amesema Zitto

Amesema watatumia mifano halisi kwenye kata husika na kutoa sera mbadala kwa misingi ya Azimio la Tabora.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527