JESHI LA POLISI LACHUKUA SIMU YA ZITTO KABWE KWA UCHUNGUZI

Simu ya mkononi ya Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe imechukuliwa na vyombo vya dola kwa uchunguzi dhidi ya tuhuma zinazomkabili.


Zitto ambaye ni Mbunge wa Kigoma Mjini, anatuhumiwa kwa makosa ya sheria ya mitandao na takwimu.

Mbunge huyo leo Jumanne Novemba 7,2017 amefika kitengo cha uhalifu wa makosa ya kifedha kilichopo Kamata, Kariakoo jijini Dar es Salaam kujua hatima yake.

Akizungumza na waandishi wa habari nje ya ofisi hizo, Zitto amesema, ''Nimeambiwa nirudi hapa Novemba 21,2017 lakini wamechukua simu yangu wanadai niliitumia kusambaza taarifa za takwimu nami nimewaachia kwa kuwa wana haki hiyo."

Amesema, "Kwa sasa sitapatikana, watu waliokuwa wananitafuta hawatanipata, kwa hiyo ndio hivyo wameamua wao lakini niwahakikishie tu kuwa mawasiliano niliyokuwa nayafanya yanalinda uhuru wangu wa Kikatiba."

Zitto amesema kabla ya kuwapatia simu walijadiliana kuhusu uamuzi huo lakini mwisho akaona awaachie wafanye wanavyotaka wao.

Amesema upekuzi pia utafanyika katika ofisi za ACT-Wazalendo na haijajulikana utafanyika lini.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527