KUTOKANA na kashifa kubwa sana inayowakabili baadhi ya Mawaziri na Wabunge wa chama cha mapinduzi (CCM) ya kuchota zaidi ya Bilioni 300 kwenye akaunti ya Tegeta Escrow baadhi ya wananchi Mkoani Geita wametakiwa kutowapa dhamana ya uongozi wenyeviti wa serikali za mitaa wanaotokana na CCM Bali wachague wenyeviti wa CHADEMA ili kuweza kuwadhibiti wezi hao kuanzia chini.
Kauli hiyo
imetolewa jana na mjumbe wa Mkutano mkuu Taifa Chadema,Tecla Johaness kwenye mkutano
wa hadhara wa kampeni wa kuwanadi wagombea wawili kupitia Chadema wa mtaa wa
Elimu,Ezekiel Matesa na mgombea wa mtaa wa Uwanja, Joseph Msoma.
Mkutano huo uliofanyika katika kiwanja cha shule ya msingi Nyankumbu ulihudhuriwa na mamia ya wananchi
ukiwa ni mwendelezo wa
mikutano inayofanywa na Chadema katika Jimbo la Geita kunadi wagombea wa
uenyekiti wa mitaa,vitongoji na vijiji.
Tecla alisema
endapo wananchi wa Tanzania wakiwachagua wenyeviti wengi wa CHADEMA kuliko wa CCM wataweza kudhibiti wizi unaondelea hata kwenye baadhi ya Halmshauri kwani viongozi wa CHADEMA ni watetezi wa wanyonge kama wanavyoona Bungeni.
“Jamani
nawaomba wananchi wangu wote wachagueni wagombea hawa waliojitokeza kupitia
CHADEMA, najua wote wana uwezo wa kutosha wa kuweza kutatua shida zenu na
kupambana na wizi unaoendelea katika taifa letu” alisema Tecla.
Katika hatua nyingine Tecla alimtaka Rais wa Jamhuri ya Tanzani Jakaya Mrisho Kikwete
kuwafukuza kazi mawaziri wawili ambao ni
Anna Tibaijuka na Sospeter Muhongo kutokana na kuiba pesa nyingi kwenye akaunti ya Tegeta Escrow ambazo ni kodi za wananchi.
Kwa upande
wake Ezekiel Matesa anayegombea mtaa wa Elimu katika kata mpya ya Nyankumbu
alisema kuwa, endapo atapewa dhamana ya kuongoza mtaa huo atahakikisha uwanja wa
shule ya msingi Nyankumbu uliouzwa na CCM unarudishwa mara moja kutokana na
wanafunzi hao wa Nyankumbu kukosa pa kuchezea.
Kwa upande
wa tatizo la umeme ambalo limekuwa kero kubwa kwa wananchi wa mtaa huo japo upo katikati ya mji wa Geita, huku aliyekuwa mwenyekiti wa mtaa huo kupitia CCM
akizidi kutoa huduma hiyo kwa gharama
kubwa kwa kutumia Jenereta alisema wananchi wameshindwa kumudu gharama hivyo kuahidi kulifanyia kazi.
Naye mgombea
wa mtaa wa Uwanja,Joseph Msoma alisema kuwa atapambana na tatizo la maji na
upimaji wa viwanja katika mtaa wake.
Pia alidai kuwa kuna tatizo la ukosefu wa umeme maana umeishia mtaa jirani wa Mbugani.
Pia alidai kuwa kuna tatizo la ukosefu wa umeme maana umeishia mtaa jirani wa Mbugani.
Uchaguzi wa
serikali za mitaa utafanyika 14 Desemba 2014 huku Jimbo la Geita likionekana
Chadema kuikaba vikali chama cha mapinduzi katika uchaguzi huo.
Na Valence Robert-Malunde1 blog- Geita
Habari za Mapenzi,Simulizi za Mapenzi na Visa vya Mapenzi utazipata Kwa Kubofya Hapa
Habari za Mapenzi,Simulizi za Mapenzi na Visa vya Mapenzi utazipata Kwa Kubofya Hapa
Social Plugin