Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

MKOA WA SHINYANGA WAPUNGUZA MAAMBUKIZI YA VVU,USHETU YATAJWA KUWA NA MAAMBUKIZI MAKUBWA

Mkuu wa Mkoa akizungumza na wananchi waliohudhuria katika maadhimisho  ya siku ya UKIMWI  duniani katika viwanja vya shule ya msingi Lunguya katika kijiji cha Lunguya wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga-picha na Magdalena Nkulu ofisi ya mkuu wa mkoa wa Shinyanga
Imeelezwa kuwa  mkoa wa  Shinyanga umefanikiwa kupunguza  maambukizi ya Ukimwi kwa kufikia kiwango cha 5.1% sawa na  asilimia 0.89 ukilinganisha na  takwimu ya mwaka  jana  ambapo maambukizi yalikuwa  ni 5.9% huku halmashauri ya Ushetu ikiongoza  kwa kuwa na idadi kubwa ya maambukizi ambayo  6.6%.

Akizungumza kwenye maadhimisho ya siku ya Ukimwi duniani Desemba mosi mwaka huu, Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Ali Nassoro Rufunga alisema  takwimu hiyo ni kwa kuanzia Januari hadi  Oktoba mwaka huu, ambapo lengo ni kufanikisha  malengo ya taifa ya kufikia sifuri tatu,                  (maambukizi mapya ya Ukimwi, Vifo vitokanavyo na Ukimwi na Unyanyapaa) ifikapo mwaka 2025

Alisema  Hali hiyo imetokana na  viongozi kuendelea kuwaelimisha  wananchi kujitokeza kwa hiali  kupima afya zao pamoja na kupewa ushauri wa kujikinga na  maambukizi pamoja na kutoa ushauri kwa wale wanaogundulika wameambukizwa  na kwamba mkoa wa shinyanga utaendelea kutoa elimu hiyo kwa wananchi wote.

Akitoa  takwimu ya Maambukizi ya Ukimwi kwa mkoa wa Shinyanga  amesema, Halmashauri ya Ushetu inaoongoza  kwa kuwa na kiwango kikubwa cha maambukizi ambayo yanafikia 6.6% Shinyanga 5.9%, Kahama mji 5.2. Kishapu 4.9,  Msalala 4.8 na Manispaa ya Shinyana 2.7%

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Msalala amapo maadhimisho ya Siku ya Ukimwi yalifanyika Zabron Donge  katika taarifa yake alisema  maeneo yanayoongoza kwa  kuwa na maambukizi ya Ukimwi  ni Maeneo ya  machimbo  kutokana na mwingiliano wa watu.

Alisema, Kijiji cha Kalole Kata ya Lunguya ambapo kuna wachimbaji wadogo  kuna idadi kubwa ya maambukizi ya ukimwi ambapo  katika kampeni ya upimaji iliyofanyika hivi karibuni  watu 485 walipima ambapo watu 32 waligundulika kuwa na maambukizi sawa na asilimia 6.6.

Aidha  aliyapongeza mashirika yasiyokuwa ya kiserikali likiwemo Shirika la Intrahearth, Kiwohede, Huheso Foundation na asasi za dini  kwa kuendelea kutoa  elimu kwa wananchi juu ya ukimwi pamoja na kuwawezesha kiujasiliamali  watu wanaoishi mazingira hatarishi.

Na Ndalike Sonda-Kahama

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com