Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

KAMPUNI YA ACACIA SASA KUWEKA TAA ZA KUONGOZEA MAGARI BARABARANI MJINI KAHAMA



Kampuni ya ACACIA kupitia mgodi wake wa Buzwagi  unatarajia kuanza kuweka taa za barabarani  pamoja na Taa za kuongozea magari katika barabara zote za Lami ambazo mgodi huo  imejenga  pamoja na maeneo mengine muhimu katika mji wa Kahama mkoani Shinyanga.
Akizungumza wakati wa kutambulisha jina  ACACIA, meneja wa mgodi wa dhahabu wa Buzwagi Filbert Rweyemamu, alisema ujenzi huo utatekelezwa ndani ya Miaka miwili  ambapo hali hiyo itasaidia  mji wa kahama kuwa na madhali nzuri nyakati za usiku.
Aidha alisema  wao  kama sehemu ya jamii   watahakikisha mji wa kahama wanaweka taa za kuongoza magari (Traffic Lights) kutokana na  mji huo kuwa na ongezeko kubwa la msongamano wa magari, pikipiki na watembea kwa miguu, na kwamba wataendelea kusaidia katika shughuli zingine za maendeleo.
Rweyemamu alipongeza serikali ya wilaya ya Kahama, kwa kukubali barabara  mojawapo iitwe jina la Kampuni (ACACIA ROAD) ambapo barabara hiyo zamani ilijulikana kama Zongomela Road, hivyo ni faraja kwao kama wahisani wakuu wa barabara hizo za lami zenye urefu wa kilomita 5.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kahama Benson Mpesya alisema Kufanikishwa kwa taa za barabarani na zile za Kuongozea magari itakuwa faraja kubwa kwa wakazi wa mji huo kwani watanufaika kwa kuppunguza msongamano na ajali zisizo za lazima.
Alisema  Mji wa Kahama utakuwa wa kwanza kupatiwa taa za kuongozea magari  hapa nchini kutokana na taa hizo mara nyingi kuwekwa katika miji mikubwa pekee hivyo waqnanchi hawana budi kuendelea kuwaunga mkono wahisani hao
“Ndugu wananchi nipende kuwapongeza ACACIA Kwa kukubaliana na ombi langu la kuweka taa katika barabara zote za lami, sasa taa za trafiki zinawekwa na ACACIA, hii itakuwa historia mji wa kahama kuwa na taa za Kuongoza magari hapa nchini , Tuzidi kuwaunga mkono watuasidie kupiti mfuko wao wa maendeleo.”alisema Mpesya.
Katika utambulisho huo wa Jina la ACACIA ambapo awali ilijulikama Kampuni ya Uchimbaji wa Madini ya Dhahabu African Gold- ABG, uongozi wa ACACIA  ukiongozwa na Afisa Mtendaji Mkuu Blad Gordon ulitembelea baadhi ya Miradi ikiwemo kutembelea barabara za lami mjini Kahama na kituo cha afya kilichopo  kata ya Mwendakulima ambapo mgodi wa Buzwagi ulipo na kupanda  miti aina ya ACACIA (Kiswahili Mgunga).
 BOFYA HAPA TUKUCHEKESHE LEO

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com