WAZIRI MWAKYEMBE AMTEMBELEA MZEE MAJUTO MUHIMBILI

Waziri Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison G. Mwakyembe (Mb) jana tarehe 23 Juni, 2018 amemtembelea msanii nguli wa filamu Bw. Amri Athumani (Mzee Majuto) ambaye amefikia katika Hospitali ya Muhimbili, Dar es Salaam akitokea India alipopelekwa na Serikali kwa ajili ya kupata matibabu.


"Serikali inafuatilia matibabu yako kwa ukaribu, hivyo usiwe na wasiwasi", alisisitiza Dkt. Mwakyembe akiongoea na Mzee Majuto. 

Akizungumza Mzee Majuto ameishukuru Serikali kwa kumhudimia na kumpeleka India kupata matibabu.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527