RED BULL WAMTABIRIA RICCIARDO


Dereva Daniel Ricciardo wa timu ya Red Bull

Mkurugenzi wa timu ya magari ya Red Bull Christian Horner, ameeleza kuwa pamoja na kuwa mkataba wa dereva kinara wa timu hiyo Daniel Ricciardo, kuelekea mwisho lakini hawategemei kumuona akiondoka licha ya kuhitajiwa na timu zingine.

Bosi huyo wa Red Bull ameyasema hayo kufuatia mashabiki wengi wa timu hiyo, kuhoji kuhusu uongozi kushindwa kutoa tamko wakati mkataba wa mkali huyo wa magari unamalizika mwishoni mwa mwaka huu.

''Ricciardo amekuwa dereva mzuri na amefanikiwa akiwa na sisi hivyo tunatarajia kumuona akiwa na sisi kwa muda mrefu zaidi lakini hatuwezi kukataa kuwa kuna ofa nyingi amepokea kutoka McLaren na Renault na zaidi sasa kuna ofa mpya kutoka Mercedes na Ferrari, uamzi ni wake lakini tutashangaa akiondoka'', amesema Horner.

Katika mbio za Formula 1 msimu huu, Ricciardo anashika nafasi ya 4 akiwa na alama 84 huku pia akiwa amefanikiwa kuongoza kwenye mbio za Monaco Grand Prix pamoja na Chinese Grand Prix.

Formula 1 inaendelea kesho ambapo zitafanyika nchini Ufaransa zikifahamika kama 'French Grand Prix'. Baadae leo zitafanyika mbio za kuwania nafasi ya kupanga gari kesho wakati wa mbio hizo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527