RAIS MAGUFULI AMEFANYA UTEUZI HUU LEO MEI 14

Rais wa Jamnhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli amemteua Prof. Siza Donald Tumbo kuwa mwenyekiti wa Bodi ya Utawala ya Chuo cha Ufundi Arusha (Arusha Technical College).

Taarifa hiyo iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Gerson Msigwa imesema kuwa uteuzi huo umeanza rasmi leo Mei 13.

Kabla ya uteuzi wa leo Prof Tumbo alikuwa Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha zana za Kilimo na Teknolojia Vijijini (Center for Agriculture Mechanization and Rural Technology - CAMARTEC).

Wakati huo huo Rais Magufuli amemteua Mhandisi Mussa Iyombe kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527