Gazeti la Mwananchi latakiwa kuomba radhi


Serikali imesema kuwa deni la jumla la taifa liliongezeka kwa Sh trilioni 3 katika kipindi cha miezi mitatu kuanzia Desemba hadi Machi mwaka huu.

Hayo yamejiri mara baada ya Gazeti la Mwananchi kutoa taarifa zisizo sahihi kuhusu deni hilo ambapo Serikali imetaka kupuuzwa kwa taarifa hiyo.

Aidha, Mkurugenzi wa Idara ya Habari-Maelezo na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi amelitaka gazeti la mwananchi kuomba radhi kwa umma kwa siku mbili mfululizo kuanzia Jumapili kupitia ukurasa wa mbele wa gazeti hilo na kwenye mitandao ya kijamii.

Hata hivyo, Dkt Abbas ameongeza kuwa baada ya gazeti hilo kusisitiza kuwa hawana nia mbaya, serikali imezingatia utetezi huo na inawapa nafasi ya kujirekebisha zaidi.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527