LADY JAYDEE AFIWA NA MAMA YAKE MZAZI

Mama mzazi wa msanii wa muziki wa bongo fleva Judith Wambura maarufu kama Lady Jaydee, Bi. Martha Mbibo, amefariki dunia alfajiri ya leo.

Akithibitisha taarifa hizo kaka wa Lady Jaydee ambaye pia ni msanii Dabo, amesema kwamba mama yao amefariki akiwa nyumbani kwake baada ya kuugua saratani kwa muda mrefu.

Dabo amesema msiba upo nyumbani kwa marehemu Jet jijini Dar es salaam, na familia itatoa utaratibu wa mazishi mara baada ya utaratibu wa kuupeleka mwili hospitali kuhifadhiwa kukamilika.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527