MBOWE ARUHUSIWA KUTOKA KCMC


Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe aliyekuwa amelazwa katika Hospitali ya Rufaa KCMC akisumbuliwa na maumivu makali ya kichwa, ameruhusiwa.

Ofisa Habari wa KCMC, Gabriel Chisseo amesema leo Jumatatu Februari 5, 2018 kuwa Mbowe ameruhusiwa baada ya madaktari kuridhishwa na afya yake iliyorejea katika hali ya kawaida.
Mbowe alikuwa amelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC akisumbuliwa na maumivu makali ya kichwa.

Chisseo amesema walimpokea Mbowe jana jioni Machi 4, 2018 akiwa na maumivu makali ya kichwa.

Amesema hali ya Mbowe inaendelea vizuri na amepumzishwa hospitalini hapo.

"Jana jioni tulimpokea Mbowe, taarifa zinaonyesha alikuwa na maumivu ya kichwa. Taarifa za kitabibu zinaonyesha ni uchovu," amesema Chisseo.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527