AJALI YA HIACE,LORI YAUA WATU 24 PWANI


Watu 24 wamefariki na wengine 10 wamejeruhiwa kwa ajali baada ya gari aina ya hiace kugongana na lori katika kijiji cha Mparanga wilayani Mkuranga mkoani Pwani.

Kaimu kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Kibiti, Mohamed Likwata amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema kwamba ajali imetokea usiku wa kuamkia leo Machi 25, baada ya hiace hiyo kugongana uso kwa uso na lori lililokuwa likitokea koani Mtwara kuelekea Dar es salaam.

Kamanda Likwata amesema majeruhi wote wamepelekwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam kwa matibabu.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527