MUME ACHINJA MKEWE UGOMVI WA ARDHI TARIME



Mkazi wa kijiji cha Kitagasembe Kata ya Gwitiryo Wilaya Tarime Mkoani Mara aliyefahamika kwa jina la Bhoke Mwita ameuawa kwa kukatwa shingo upande wa kulia kwa kitu chenye ncha kali na mumewe Mwita Mganya kwa kumkataza asiuze ardhi.

Kaimu kamanda wa polisi Tarime Rorya Obadia Jonas amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba mtuhumiwa baada ya kutekeleza unyama huo alitokomea kusikojulikana na jeshi la polisi linafanya kila juhudi kuhakikisha linamtia nguvuni.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Kitagasembe Gabriel Mnanka alisema chanzo mauaji hayo ni migogoro ya ardhi kati mtuhumiwa na marehemu baada ya marehemu kukataa mumewe asiuze ardhi ya familia ndipo aliamua kufanya unyama huo

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527