BABU SEYA, PAPII KOCHA WATOKA GEREZANI....HAWA HAPA

Mwanamuziki Nguza Viking ‘Babu Seya’ na mwanaye Johnson Nguza ‘Papii Kocha’ wametoka katika gereza la Ukonga jioni hii baada ya kusota kwa miaka 13.

Wanamuziki hao ‘baba na mwana’ walitoka katika kifungo cha maisha baada ya kupata msamaha wa Rais John Magufuli leo Jumamosi Desemba 9, mwaka 2017.

JPM alitoa msamaha kwa baadhi ya wafungwa alipokuwa akihutubia Taifa kusherehea miaka 56 ya Uhuru wa Tanzania Bara na miongoni mwa waliopata ahueni hiyo ni Babu Seya na Papii Kocha.

“Babu, babu, babu,” zilikuwa ni kelele za mashabiki na ndugu zake waliompokea Babu Seya na Papii Kocha waliokuwa wametoka gerezani wakiwa na magitaa yao mgongoni.

Babu Seya aliyeonekana mtanashati alionekana anapunga mkono wa kulia kama mtu asiyeamini huku Papii Kocha akipunga mkono akionekana kufurahia na kuzungumza na mashabiki.

Walisindikizwa na askari magereza mpaka nje na kulikuwa na foleni kubwa kutokana na tukio hilo.
Chanzo- Mwananchi
</div>

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527